Home » Tanzania » UMOJA WA ULAYA WAIPATIA TANZANIA MSAADA WA SHILINGI BILIONI 130 KUSAIDIA UPATIKANAJI UMEME VIJIJINI

UMOJA WA ULAYA WAIPATIA TANZANIA MSAADA WA SHILINGI BILIONI 130 KUSAIDIA UPATIKANAJI UMEME VIJIJINI

03 November 2017 | Tanzania
 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi Amina Shaban (kushoto) akiupokea ujumbe kutoka Umoja wa Ulaya, ukiongozwa na Kamishna wa Ushirikiano wa Kimataifa na Maendeleo Bw. Neven Mimica (katikati) na Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania Bw. Roeland van de Geer, walipokuwa wanawasili Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa msaada wa Euro milioni 50 kwa Tanzania.
 
 
Ujumbe kutoka Umoja wa Ulaya pamoja na Maafisa wa Wizara ya Fedha na Mipango wakimsikiliza kwa makini, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James akitoa maelezo ya ujio wa ugeni huo kuwa ni neema kwa nchi ya Tanzania kwani Umoja wa Ulaya wametoa msaada wa Euro Milioni 50 utasaidia vijijini 3600 nchini kupata umeme.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James (kulia) na akimweleza jambo Kamishna wa Ushirikiano wa Kimataifa na Maendeleo wa Umoja wa Ulaya Mr. Neven Mimica wakati wa hafla fupi ya Umoja wa Ulaya (EU) kutiliana saini makubaliano ya msaada wa Euro milioni 50 kwa ajili ya kusaidia usambazi wa umeme vijijini kupitia Mradi Kabambe wa Kusambaza umeme Vijijini (REA).
Ad