Home » Nje Ya Afrika » SERIKALI ya Jamhuri ya Poland mapema mwezi April mwaka huu inatarajia kufungua upya Ofisi za Ubalozi

SERIKALI ya Jamhuri ya Poland mapema mwezi April mwaka huu inatarajia kufungua upya Ofisi za Ubalozi

23 February 2018 | Nje ya Afrika

 

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais wa Poland Mhe. Krzysztof Szczerski  wakati alipoleta salamu za Rais wa Poland na mwaliko kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli, mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe (kulia) akipokea salamu za Rais wa Poland na mwaliko kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli toka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais wa Poland Mh.Krzysztof Szczerski.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais wa Poland Mh.Krzysztof Szczerski (kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe mara baada ya kukabidhi  salamu za Rais wa Poland na mwaliko kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe (kulia) akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais wa Poland Mh.Krzysztof Szczerski wakati alipoleta salamu za Rais wa Poland na mwaliko kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe (kushoto) akifurahia jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais wa Poland Mh.Krzysztof Szczerski  mara baada ya kupokea salamu za Rais wa Poland na mwaliko kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe (kushoto) akisalimiana na Balozi wa Poland nchini Tanzania Mh. Krzysztof Buzalski mapema hii leo jijini Dar es Salaam wakati walipoleta salamu na mwaliko wa Rais wa Poland kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli, Waziri Mwakyembe aliokea salamu hizo kwa niaba ya Rais Magufuli. Picha zote na Eliphace Marwa – MAELEZO
 
Na Ismail Ngayonga
SERIKALI ya Jamhuri ya Poland mapema mwezi April mwaka huu inatarajia kufungua upya Ofisi za Ubalozi wa nchi hiyo hapa nchini ambazo zilifungwa kwa muda, hatua inalenga kuimarisha uhusiano na ushirikiano baina ya Mataifa hayo.
 
Hayo yamesemwa leo Ijumaa (Februari 23, 2018) Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe wakati alipokuwa Salamu za Rais wa Poland kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.
 
Dkt. Mwakyembe alisema hatua zote muhimu za ufunguzi wa Ubalozi huo, taratibu zote muhimu kwa ajili ya ufunguzi Ofisi za Ubalozi huo tayari zimekamilika na kuongeza kuwa kufunguliwa kwa ubalozi kutazidi kudumisha ushirikiano na urafiki wa muda mrefu baina ya Tanzania na Poland pamoja na kuimarisha diplomasia ya uchumi baina ya mataifa hayo.
 
 “Serikali ya Jamhuri ya Poland imekuwa na ushirikiano wa muda mrefu na Tanzania, ambapo matunda ya ushirikiano ni kwa Serikali yetu kupata wa mkopo wa masharti nafuu uliofanikisha uanzishaji wa kiwanda kikubwa cha matrekta kibaha Mkoani Pwani” alisema Dkt. Mwakyekmbe.
 
Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais wa Poland Krzysztof Szczerski  alisema ziara yake ya kuja nchini ni kuwasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Poland ambapo pamoja na mambo mengine Serikali ya nchi hiyo imekusudia kuimarisha mahusiano yake ya kiuchumi na Tanzania.
 
Aliongeza kuwaa katika kuendeleza jitihada zake za kuimarisha uhusiano wake na Tanzania, Serikali ya Poland tayari inaendesha miradi mbalimbali ya uwekezaji nchini ambapo Rais wa Poland ameahidi kuimarisha ushirikiano huo baina yake na Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.
 
“Niwewasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Poland ambapo pamoja na mambo mengine, amemualika Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenda nchini Poland kwa ajili ya ziara maalum ya kiserikali” alisema Szczerski.
Ad