Home » Tanzania » Rais Magufuli atengua uteuzi wa DED Mkinga aitwaye Emmanuel Mkumbo

Rais Magufuli atengua uteuzi wa DED Mkinga aitwaye Emmanuel Mkumbo

18 October 2016 | Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga ajulikanae kwa jina la Emmanuel Mkumbo.

Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Emmanuel Mkumbo kuanzia leo tarehe 18 Oktoba, 2016.

Uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga atakayejaza nafasi ya Emmanuel Mkumbo utafanywa baadaye.

 

 

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

18 Oktoba, 2016

 

Ad