Home » Node

Chama cha kansela wa Ujerumani, Angela Merkel kimepata pigo

Chama cha kansela wa Ujerumani, Angela Merkel kimepata pigo kubwa kwenye uchaguzi wa majimbo uliofanyika hapo jana, ambapo wachambuzi wa mambo wanasema hali hiyo imetokana na sera ya chama chake kuhusu wahamiaji na wakimbizi.

Chama cha mrengo wa kulia cha AFD kimeshuhudiwa kikiweka historia kwenye uchaguzi wa safari hii, baada ya kupata kura nyingi zinazoelezwa kutoka kwa wananchi wenye hasira na sera za Kansela Merkel kuhusu wahamiaji.

Jeshi la Afrika Kusini limekashifu shambulio wanajeshi wa kulinda amani Darfur

Jeshi la Afrika Kusini limekashifu vikali shambulio la kushtukiza lililotekelezwa kuwalenga wanajeshi wake wa kulinda amani kaskazini mwa jimbo la Darfur nchini Sudan, na kuongeza kuwa kitendo hicho hakikubaliki.

Jeshi la Afrika Kusini limetoa kauli hii wakati huu likithibitisha kuwa wanajeshi wake wawili waliuawa juma lililopita kwenye shambulio la kushtukiza na kuwataja waliouawa kwenye shambulio hilo kuwa na Koplo Msolisi Edward na Brigedia Jenerali Solani Mabanga.

Wanajeshi walioasi kwenye jeshi la Sudan Kusini kwenye majadiliano na utawala wa Juba

Hatimaye wanajeshi walioasi kwenye jeshila Sudan Kusini na kwenda kupigana sambamba na aliyekuwa makamu wa rais Riek Machar, wamewasili mjini Juba wakimaliza miezi kadhaa ya majadiliano na utawala wa Juba.

Miongoni mwa waliowasili mjini Juba hapo jana ni pamoja na aliyekuwa jenerali wa jeshi la Sudan Kusini kabla ya kuasi, Jenerali, Gathoth Gatkuoth, james Malith Gatluak, Chuol Gakah na Gabriel Yoal Dok, mwenyekiti wa kabila la Nuer walioambatana na wapiganaji wao.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS