VIDEO: Dkt. John Pombe Magufuli amemtembelea Seif Shariff Hamad
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtembelea na kumjulia hali Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Maalim Seif Shariff Hamad, katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam, ambako anapata mapumziko baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali ya Hindu Mandal alikokuwa amelzwa kwa matibabu.
Pamoja na kumpa mkono wa pole, Rais Magufuli amemuombea Maalim Seif Shariff Hamad kupona haraka ili aweze kuendelea na shughuli zake kama kawaida.
Dkt. Magufuli amemtembelea na kumjulia hali Maalim Seif Shariff Hamad
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtembelea na kumjulia hali Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Maalim Seif Shariff Hamad, katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam, ambako anapata mapumziko baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali ya Hindu Mandal alikokuwa amelzwa kwa matibabu.

Polisi mmoja nchini Zimbabwe kujibu mashtaka ya kumdhalilisha rais Mugabe
Polisi mmoja nchini Zimbabwe amefikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kumdhalilisha rais kwa kudai kuwa ni mzee sana kuongoza huku akimfananisha mke wake na wasichana wanaofanya biashara ya ngono.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Zimbabwe, vimeripoti kuwa, polisi huyo, Thompson Joseph Mloyi, amekana mashtaka dhidi yake, ambapo anadaiwa kuwa alitoa maneno ya kejeli dhidi ya rais Mugabe na mke wake, akiwa kwenye kambi moja ya jeshi na polisi.
Upinzani nchini Niger umesema kuwa hautashiriki Duru ya pili
Upinzani nchini Niger umesema kuwa hautashiriki Duru ya pili ya uchaguzi wa rais ambao umepangwa kufanyika tarehe 20 mwezi huu wa Marchi.
Uchaguzi huu utafanyika wakati Hama Amadou, hasimu wa Rais Mahamadou Issoufou wa Niger katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais nchini humo, bado anaendelea kushikiliwa na vyombo vya dola licha ya kukaribia uchaguzi huo.
Francois: jitihada za ziada zinahitajika kuharakisha kusaka ufumbuzi libya.
Jeshi la Tunisia limewekwa katika hali ya tahadhari baada ya kutokea kwa mashambulizi ya kigaidi katika mji wa Ben Guerdan ulioko karibu na mpaka wa pamoja wa nchi hiyo na Libya ambapo iliarifiwa kuwa Watu 53 waliuawa.
Moise Katumbi alaani polisi cha kuvamia Kanisa la Basilica St Mary jana mjini Lubumbashi
Gavana wa zamani wa mkoa wa Katanga, Moise Katumbi amesema kuwa hakufurahishwa na kitendo cha polisi cha kuvamia Kanisa la Basilica St Mary jana mjini Lubumbashi, wakati alikuwa akishiriki ibada iliyoandaliwa katka muktadha wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake.
Jeshi la Marekani imeeleza kuwa Kiongozi wa kundi IS Omar le Tchetchen ameuawa
Jeshi la Marekani imeeleza kuwa Kiongozi wa kundi linalojiita Islamic State Omar al-Shishani, maarufu kama Omar le Tchetchen ameuawa katika mashambulizi ya anga yaliotekelezwa mwishoni mwa juma lililopita.
Taarifa hiyo ya jeshi la Marekani inasema huenda kiongozi huyo ameuawa na wapiganaji wemngine 12 wa kundi hilo katika mashambulio ya anga yaliotumiwa ndege zisizokuwa na rubani pamoja na ndege nyingine za kivita.












