Home » Node

VIDEO: Dkt. John Pombe Magufuli amemtembelea Seif Shariff Hamad

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtembelea na kumjulia hali Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Maalim Seif Shariff Hamad, katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam, ambako anapata mapumziko baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali ya Hindu Mandal alikokuwa amelzwa kwa matibabu.

Pamoja na kumpa mkono wa pole, Rais Magufuli amemuombea Maalim Seif Shariff Hamad kupona haraka ili aweze kuendelea na shughuli zake kama kawaida.

Polisi mmoja nchini Zimbabwe kujibu mashtaka ya kumdhalilisha rais Mugabe

Polisi mmoja nchini Zimbabwe amefikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kumdhalilisha rais kwa kudai kuwa ni mzee sana kuongoza huku akimfananisha mke wake na wasichana wanaofanya biashara ya ngono.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Zimbabwe, vimeripoti kuwa, polisi huyo, Thompson Joseph Mloyi, amekana mashtaka dhidi yake, ambapo anadaiwa kuwa alitoa maneno ya kejeli dhidi ya rais Mugabe na mke wake, akiwa kwenye kambi moja ya jeshi na polisi.

Jeshi la Marekani imeeleza kuwa Kiongozi wa kundi IS Omar le Tchetchen ameuawa

Jeshi la Marekani imeeleza kuwa Kiongozi wa kundi linalojiita Islamic State Omar al-Shishani, maarufu kama Omar le Tchetchen ameuawa katika mashambulizi ya anga yaliotekelezwa mwishoni mwa juma lililopita.

Taarifa hiyo ya jeshi la Marekani inasema huenda kiongozi huyo ameuawa na wapiganaji wemngine 12 wa kundi hilo katika mashambulio ya anga yaliotumiwa ndege zisizokuwa na rubani pamoja na ndege nyingine za kivita.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS