Home » Node

Staffan de Mistura amepongeza maendeleo ya usitishwaji mapigano

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Syria Staffan de Mistura amepongeza maendeleo ya usitishwaji mapigano, lakii hata hivyo amesema hakuna dhamana ya hali hiyo kuendelea.

Hata hivyo Demistura amesema hali ilivyo kwenye uwanja wa mapambano ni tulivu, lakini ni dhaifu, hivyo hakuna dhamana ya utulivu huo kuendelea kushuhudiwa. Vikao vinaendelea kuhakikisha pande zote mbili zinaendelea kuhsimisha makubaliano.

Uteuzi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu NSSF Dkt. Carina Wangwe watenguliwa

Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mheshimiwa Jenister Joakim Mhagama ametengua uteuzi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dkt. Carina Wangwe uliotangazwa leo Jijini Dar es salaam.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa usiku huu, imeeleza kuwa uteuzi huo umetenguliwa kutokana na kutokamilika kwa baadhi ya taratibu.

Rais wa Tanzania amefanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Kenya

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta, kando ya Mkutano Mkuu wa 17 wa kawaida wa wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika Mkoani Arusha, ambapo viongozi hao wamekubaliana kuimarisha mahusiano hususani katika masuala ya kiuchumi.

Marais EAC wasaini ya Kanuni za Madili ya Mfuko wa Sekta Binafsi

Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wamemteuwa rais wa Tanzania John pombe Magufuli kuwa mwenyekiti wa Jumuiya ya hiyo katika mkutano wa 17 wa marais uliofanyika hii leo huko Arumeru Mkoani Arusha.

Akihutubia katika mkutano huo rais magufuli amesema viongozi wa Jumuiya hiyo wote kwa pamoja wamekubali ombi la Sudani Kusini kujiunga na Jumuiya hiyo.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS