Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 07 Novemba, 2017 amefungua barabara ya lami ya Kyaka – Bugene Mkoani Kagera yenye urefu wa kilometa 59.1 iliyogharimu Shilingi Bilioni 81.597 fedha zote zikiwa zimetolewa na Serikali ya Tanzania.
UMOJA WA ULAYA WAIPATIA TANZANIA MSAADA WA SHILINGI BILIONI 130 KUSAIDIA UPATIKANAJI UMEME VIJIJINI
RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AFUNGUA DARAJA LA JUU LA WATEMBEA KWA MIGUU LILILOPO FURAHISHA JIJINI MWANZA
RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE.DKT.JOHN POMBE MAGUFULI AFUNGUA VIWANDA VIWILI MKOANI MWANZA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 31 Oktoba, 2017 amefungua kiwanda cha kuzalisha bidhaa za plastiki cha Victoria Moulders na kiwanda cha dawa za binadamu cha Prince Pharmaceuticals Co. Ltd vilivyopo katika wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza.
Uchaguzi mdogo wa Udiwani katika Kata 43 kufanyika Novemba 26 mwaka huu
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 43 kuwa utafanyika Novemba 26 mwaka huu.
Mwenyekiti wa NEC Jaji Semistocles Kaijage, amesema kuwa uchaguzi huo unafanyika kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo baadhi ya madiwani kufariki dunia, kujiuzulu, kutohudhuria vikao na wengine ushindi wao kutenguliwa na Mahakama.
RAIS DKT MAGUFULI AWAAPISHA MABALOZI WAPYA WA TANZANIA NCHINI MISRI NA ZAMBIA
RAIS DKT MAGUFULI AWAAPISHA MABALOZI WAPYA WA TANZANIA NCHINI MISRI NA ZAMBIA
YALIYOJIRI BUNGENI KATIKA KIPINDI CHA MASWALI NA MAJIBU - SEPTEMBA 13, 2017.
#WizarayaAfya hadi sasa imesambaza vifungashio 60,000 kwa mikoa 6 ya kanda ya Ziwa - Dkt. Hamisi Kigwangala.
#Ni jukumu la kila Halmashauri kuweka mahitaji ya vifungashio (delivery pack) - Dkt. Hamisi Kigwangala.
UWASILISHWAJI WA MUSWADA WA SHERIA YA RELI YA MWAKA 2017 (THE RAILWAY ACT, 2017)
#Muswada unapendekeza kutungwa kwa sheria itakayoanzisha Shirika la Reli Tanzania (TRC) ambalo litakuwa na jukumu la kusimamia, kuendeleza miundombinu ya reli na kutoa huduma ya usafiri wa reli - Prof. Makame Mbarawa.
Rais John Magufuli ameivunja Mamlaka ya Usimamizi wa Mji Mdogo wa Kigamboni (KDA)
Rais John Magufuli ameivunja Mamlaka ya Usimamizi wa Mji Mdogo wa Kigamboni (KDA) na sasa shughuli zake zinahamishiwa katika Manispaa ya Kigamboni.
Akizungumza leo Jumatano,Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amesema ametumwa na Rais Magufuli kutangaza uamuzi huo.
"Kumekuwa na mgongano katika usimamizi wa ardhi kati ya KDA na Manispaa ya Kigamboni, Rais ameliona hilo na kuamua kuivunja mamlaka hiyo,"amesema.
TRA Yaanza Kukusanya Kodi Kwenye Michezo ya Kubahatisha
Na: Thobias Robert
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeanza rasmi kukusanya kodi kwenye michezo ya kubahatisha kama ambavyo ilikabidhiwa jukumu hilo kuanzia Julai Mosi 2017 kwa mujibu wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2017.


















