Home » Node

Makamu wa Rais "Miradi yote yenye thamani isiyozidi bilioni 10 wapewe Wakandarasi wa ndani"

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ameagiza kuwa miradi yote yenye thamani isiyozidi bilioni 10 wapewe Wakandarasi wa ndani hasa kwa miradi inayotekelezwa kwa fedha za ndani kwani wakandarasi hao watasaidia kuongeza ajira kwa vijana wa Kitanzania na kuongeza uwekezaji ndani ya nchi.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo mjini DODOMA wakati anafungua mkutano wa siku Mbili wa mashauriano wa Bodi ya Usajili wa Wakandarasi mwa mwaka 2017.

HAFLA YA KUKABIDHIWA RIPOTI YA VYETI FEKI

Viongozi mbalimbali wa kitaifa wameshaingia kwenye ukumbi wa Chimwaga. Yupo Katibu Mkuu Kiongozi, Waziri wa Utumishi, Mh. Angeka Kairuki, Waziri wa Elimu Prof. Ndalichako, Spika wa Bunge la JMT, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Waziri Mkuu wa JMT, Makamu wa Rais na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameshaketi meza kuu.

Kwa ufupi Serikali yote ipo Chimwaga.

Rais Magufuli ameshawasili na wimbo wa Taifa umeimbwa.

Mama Samia Suluhu ameanza kuwasalimia wanafunzi wa UDOM.

13 watakiwa waripoti na Mitambo ya Kurudufu CD Polisi Centre - RC DSM

Baadhi ya wasanii wa Filamu nchini (Bongo Movie) wamefanya maandamano katika Mtaa wa Aggrey, Kariakoo ambapo ni sehemu maarufu kwa kuuza kazi za sanaa (CD za filamu mbalimbali) za ndani na nje ya nchi.

Wasanii hao wamefikia uamuzi huo ikiwa ni kupinga uingizwaji wa filamu kutoka nje ya nchi ambazo wamedai kuwa zinaporomosha soko la filamu za ndani hivyo kusababisha kazi zao zisifanye vizuri sokoni.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS