Home » Node

"Madaktari 258 ambao waliokuwa waende Kenya, sasa waajiriwe Tanzania " JPM

Mnamo tarehe 18 Machi 2017 Ujumbe wa Serikali ya Kenya ukiongozwa na Waziri wa Afya Dkt. Cleopa Mailu uliwasili nchini ambapo ulikutana na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

Dhumuni la mkutano huo ulikua kuomba kuajiri, kwa Mkataba, Madaktari wa Tanzania mia tano (500), ili kupunguza uhaba wa Madaktari nchini Kenya.

Mheshimiwa Rais JPM, alikubali ombi hilo.

Bunge la nchi hiyo limeunga mkono hoja ya Waziri Mkuu Theresa May ya kufanya uchaguzi wa mapema

Siku moja baada ya Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May kuitisha uchaguzi wa Mapema, hatimaye Bunge la nchi hiyo limeunga mkono hoja ya Waziri Mkuu Theresa May ya kufanya uchaguzi wa mapema. Sasa uchaguzi Mkuu wa Uingereza utafanyika Juni 8 , 2017.

Theresa May, ametaka idhini kutoka kwa raia wa Uingereza katika kuendeleza mazungumzo ya mchakato wa Uingereza kuondoka Muungano wa Ulaya.

TTCL yazindua kampeni ya “NJOO NYUMBANI HUKO ULIKO SIO KWENU”

TTCL yazindua kampeni ya “NJOO NYUMBANI HUKO ULIKO SIO KWENU"

Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) imezindua kampeni  mpya ya kuhamasisha watumiaji wa simu za mkononi kujiunga na mtandao wa TTCL ulio boreshwa kwa kasi ya 4G LTE wakiwa na kauli mbiu ya ‘Njoo Nyumbani Huko uliko sio kwetu’.

Mteja atakapo nunua kifurushi chochote cha TTCL anapata BURE huduma za mitandao ya kijamii kama Whatsapp, facebook, twitter, Instergram na E-mail.

Rais Magufuli ateua kamati maalum ya pili ya wachumi na wanasheria kuchunguza mchanga wa madini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 10 Aprili, 2017 ameteua wajumbe wa kamati maalum ya pili itakayofanya uchunguzi wa madini yaliyomo kwenye mchanga wenye madini ulio ndani ya makontena yaliyopo katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Kamati hiyo inajumuisha wachumi na wanasheria na imetanguliwa na kamati ya kwanza iliyoundwa na wataalamu wa masuala ya jiolojia, kemikali na uchambuzi wa kisayansi.

Hafla ya kuapishwa viongozi hao imefanyika Ikulu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 05 Aprili, 2017 amewaapisha viongozi aliowateua kushika nyadhifa mbalimbali.

Hafla ya kuapishwa viongozi hao imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Dkt. Magufuli amemuapishwa Dkt. Leonard Douglas Akwilapo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Makamu wa Rais afungua maonyesho ya Kibiashara kati ya Ufaranza na Tanzania yanayofanyika Jijini Dar es Salaam

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa Tanzania ni Moja ya nchi salama kwa ajili ya uwekezaji barani Afrika kwa sababu haina matatizo ya migogoro ambayo yanaweza kuhatarisha usalama wa mali ya wawekezaji ikilinganishwa na nchi nyingine barani Afrika.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo wakati akifungua maonyesho ya Kibiashara kati ya Ufaranza na Tanzania yanayofanyika Jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli afungua kikao cha pamoja cha Mawaziri wa Serikali za Tanzania na Uganda Ikulu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli afungua kikao cha pamoja cha Mawaziri wa Serikali za Tanzania na Uganda pamoja na wadau kuzungumzia mradi wa ujenzi wa Bomba la Kusafirishia Mafuta Ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga.

Mkutano huo, uliofanyika Ikulu, Dar es salaam, Machi 28, 2017, ulihudhuriwa na Mawaziri wa Nishati na Madini pamoja na Mawaziri wa Ardhi wa nchi hizo mbili, Wanasheria wa Serikali na kampuni washirika wa mradi huo Lake Albert (CNOOC, TOTAL na TULLOW).

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS