Home » Node

Uzinduzi wa barabara ya Southern By-pass

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta leo tarehe 01 Novemba, 2016 wamezindua barabara ya Southern By-pass iliyojengwa kwa lengo la kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Nairobi nchini Kenya.

Sherehe ya uzinduzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 28 na inayounganisha maeneo mbalimbali ya Jiji la Nairobi imefanyika katika eneo la Karen nje kidogo ya Jiji la Nairobi.

Utafiti uliofanywa nchini DRCongo hivi karibuni

Utafiti uliofanywa nchini DRCongo hivi karibuni, unaonyesha kwamba asilimia 80,4 ya wananchi wa taifa hilo wanapinga muhula wa 3 wa rais Joseph Kabila, huku wengine wakiona kwamba kiongozi huyo anatakiwa kuondoka madarakani Novemba 19 mwaka huu.

Huku asilimia kubwa ikiona kwamba iwapo uchaguzi utafanyika nchini humo viongozi ambao hawakushiriki katika mjadala wa kitaifa uliofanyika nchini humo hivi karibuni

Dkt. Magufuli amesema Serikali imetenga Bii 483 kwa mwaka huu ambapo wanafunzi takribani 93,000

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 21 Oktoba, 2016 ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa mabweni 20 ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3,840 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa Mwezi Juni mwaka huu wakati wa sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa maktaba ya kisasa ya chuo hicho.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mkurugenzi LUWASA)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Lindi (LUWASA), Mhandisi Adam Alexander kwa kosa la matumizi mabaya ya ofisi pamoja na kushindwa kusimamia ujenzi wa kituo cha kuzalisha maji katika Manispaa ya Lindi.

 

Waziri Mkuu amemkabidhi Mhandisi huyo kwa Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Lindi, Bw. Stephen Chami na kumuelekeza afanye uchunguzi zaidi juu ya suala hilo.

 

Elimu ya Mpiga Kura

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa fursa kwa vyombo vya habari kuialika kutoa Elimu ya Mpiga Kura kwa Wamiliki,Wahariri na wafanyakazi wa vyombo hivyo ili kukuza uelewa juu ya sheria, kanuni, na taratibu zinazoongoza na kusimamia uendeshaji wa uchaguzi na kufahamu majukumu ya Tume hapa nchini.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Bw. Kailima Ramadhani ofisini kwake wakati akitoa tathmini juu ya Elimu ya Mpiga Kura inayotolewa na Tume hivi sasa hapa nchini.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS