Home » Node

Kizza Besigye asitangazwe LIVE

Serikali ya Uganda imepiga marufuku vyombo vya Habari nchini humo kupeperusha matangazo ya moja kwa moja maandamano ya upinzani yakiongozwa na Kizza Besigye kutoka chama cha FDC kuendelea kupinga ushindi wa rais Museveni mwezi Februari.

Hii inamaanisha kuwa vyombo vya Habari haviruhusiwi kuwahoji wanasiasa wa upinzani au kuonesha shughuli zao za kisiasa wakati huu rais Museveni akitarajiwa kuapishwa Alhamisi ijayo.

Moise Katumbi Chapwe kuchunguzwa

Siku moja baada ya Gavana wa zamani wa Jimbo la Katanga nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Moise Katumbi Chapwe kutangaza nia yake ya kuwania urais mwezi Novemba kupitia muungano wa vyma vya upinzani, serikali nchini humo imeamuru uchunguzi kufanyika dhidi ya mwanasiasa huyo kutumia mamluki kutoka Marekani kumlinda.

Hata hivyo, madai haya yamekanushwa na Katumbi ambaye amesema ni ya uongo na hawezi kutumia silaha kuingia madarakani.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS