Home » Node

Jenerali Jean-Marie Michel Mokoko, anazuiliwa na maafisa wa usalama

Mwanasiasa wa upinzani nchini Congo Brazaville aliyewania urais mwezi Machi huu Jenerali Jean-Marie Michel Mokoko, anazuiliwa na maafisa wa usalama.Ripoti zinasema hatua ya kukamatwa kwa Jenerali huyo zimekuja baada ya mwanasiasa huyo kujadili mipango ya kumwondoa madarakani rais Sassou Nguesso kwa ushrikiano na afisa wa Inteljensia kutoka Ufaransa.

Mapigano nchini Syria yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 280,000

Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani John Kerry ameionya Urusi kuwa, uvumilivu wa Marekani kuhusu vita vinavyoendelea na hatima ya raia Bashar Al Assad kuendelea kuwa madarakani unafika mwisho.

Akiwa ziarani nchini Norway, Kerry amesema ni muhimu kwa Urusi kuelekwa kuwa uvumilivu wa nchi yake una mwisho, na kusisitiza kuwa rais Assad ni lazima awajibishwe kutokana na vita vinavyoendelea tangu mwaka 2011.

Kizza Besigye anayezuiliwa kwa kosa la uhaini ashtakiwe Mahakamani

Mahakama jijini Kampala nchini Uganda, imeamua kuwa kingozi wa upinzani kutoka chama cha FDC Kizza Besigye anayezuiliwa kwa kosa la uhaini ashtakiwe Mahakamani, sio katika Gereza la Luzira kama serikali inavyotaka.

Kiongozi wa mashtaka amekuwa akishindwa kumfikisha Mahakamani Dokta Besigye kuanzia mapema mwezi huu kwa madai kuwa kufanya hivyo kutahatarisha hali ya usalama.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS