Home » Node

Vijana hawajajengewa maarifa na ujuzi wa kuajiriwa na kuajirika - Waziri Mkuu

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana nchini kimepungua kwa asilimia 2.5 na kwamba Serikali itaendeleza juhudi za kuvutia uwekezaji ili kupunguza zaidi kiwango hicho.
 
Ametoa kauli hiyo leo mchana (Ijumaa, Aprili 22, 2016) wakati akiwasilisha mapitio na mwelekeo wa kazi za Serikali na makadirio ya mapato na matumizi ya fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2016/2017 bungeni mjini Dodoma.
 

Zuma amesema uchunguzi kuhusu ununuzi wa silaha haukuwa na ufisadi

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesema uchunguzi kuhusu ununuzi wa silaha miaka ya tisini uliofanywa na serikali, umebaini kuwa haukuwa na visa vyovyote vya ufisadi.

Wapinzani wa serikali ya ANC kwa muda mrefu wamekuwa wakidai kuwa Dola Bilioni 2 nukta 1 zilizotumiwa na serikali kununua silaha hizo kununua silaha hizo kutoka jeshi kutoka Mataifa ya Ulaya, zilitumiwa vibaya na kwa sababu za kisiasa.

Sepp Blatter kumshawishi rais Piere Nkurunziza kutowania urais kwa muhula wa tatu

Rais wa zamani wa Shirikisho la soka duniani FIFA Sepp Blatter mwaka uliopita alijaribu kuwa mpatanishi katika mzozo wa Burundi kumshawishi rais Piere Nkurunziza kutowania urais kwa muhula wa tatu, lakini hakufanikiwa.

Hili nimebainika baada ya kuzinduliwa kwa kitabu kumhusu Blatter.

Blatter ameeleza katika kitabu hiki kuwa Wizara ya Mambo ya nje ya Uswizi ilimwomba kuwa msuluhishi wa mgogoro.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS