Home » Node

Serikali imetenga kiasi cha sh. bilioni 1.65/- kwenye vyuo vya walimu

'SERIKALI YATENGA SH. BILIONI 1.6/- VYUO VYA UALIMU"

 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imetenga kiasi cha sh. bilioni 1.65/- kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo kwenye vyuo vya walimu hapa nchini.

Alitoa kauli hiyo (Jumamosi, Februari 27, 2016), wakati akizungumza na walimu na watumishi wa sekta ya elimu kutoka wilaya zote za Mkoa wa Mtwara uliofanyika kwenye ukumbi wa Chuo cha Ualimu Mtwara.

VIDEO - HAYA NDIYO BAADHI YA YALIYOSABABISHA UCHAGUZI ZANZIBAR UFUTWE

HAYA NDIYO YALIYOSABABISHA UCHAGUZI ZANZIBAR UFUTWE

Baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha kuwataka waandishi wote wa habari za kiuchunguzi pamoja na watafiti kuweka hadharani na kuueleza umma kile kilichotokea Zanzibar, Waandishi na watafiti mabalimbalai wamejitokeza  na vielelezo  vinavyoeleza jinsi uchaguzi huo ulivyoharibika

HAYA NDIYO BAADHI YA YALIYOSABABISHA UCHAGUZI ZANZIBAR UFUTWE

 HAYA NDIYO YALIYOSABABISHA UCHAGUZI ZANZIBAR UFUTWE

 

Baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha kuwataka waandishi wote wa habari za kiuchunguzi pamoja na watafiti kuweka hadharani na kuueleza umma kile kilichotokea Zanzibar, Waandishi na watafiti mabalimbalai wamejitokeza  na vielelezo  vinavyoeleza jinsi uchaguzi huo ulivyoharibika

Usalama Barabarani kanda maalum ya Dar es salaam wa kusanya shilingi BILIONI (1.9)

Kikosi cha usalama barabarani kanda maalum ya Dar es salaam kimetangaza kukusanya kiasi cha shilingi BILIONI MOJA NUKTA TISA (1.9) kutokana na faini za ukamataji wa makosa ya usalama barabarani kuanzia siku ya kwanza ya February 2016 mpaka tarehe 22 ya mwezi huu.

Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es salaam Simon Sirro amesema ‘Sio kwamba tunafurahia watu wafanye makosa ili tuingize pesa, hatupendi tuwe na pesa nyingi za makusanyo kwa ajili ya kuonea Wananchi… hapana, tunafanya hivyo kudhibiti na kuhakikisha kunakuwa na utii wa sheria‘

Viongozi wa Umoja wa Afrika kuwasili nchini Burundi hiyo kesho

Viongozi wa Umoja wa Afrika wanatarajiwa kuwasili nchini Burundi hiyo kesho kama njia ya kuongeza jitihada za kumaliza mgogoro wa Burundi uliozuka mwezi April mwaka jana baada ya rais Pierre Nkurunziza kugombea urais kwa muhula wa tatu.

Ujumbe wa Umoja wa Afrika unaongozwa na rais wa Afrika Kusini Jakob Zuma na utakuwa nchini Burundi kwa siku mbili katika harakati hizo za kusaka amani nchini Burundi.

Viongozi wengine waliopo katika ujumbe huo ni 

Ban Ki Moon ametembelea kambi za watu waliokimbia makazi yao mashariki mwa DRC

Katibu mkuu wa umoja wa Mataifa Ban Ki Moon ametembelea kambi za watu waliokimbia makazi yao mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo, DRC na kueleza hatua ambazo Umoja wa Mataifa utachukua kukabiliana na hali hiyo.

Ban Ki Moon amesema kuwa matatizo yanayowakumba raia wa mashariki mwa DRC yanapaswa kutfutiwa ufumbuzi kwa kuzingatia haki za binadamu na kuepusha mauaji ya mara kwa mara.

Rais wa Syria amemhakikishia rais wa Urusi kuheshimu makubaliano

Rais wa Syria Bashar al-Assad amemhakikishia rais wa Urusi Vladimir Putin kuhusu utayari wake wa kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa na Marekani na Urusi .

Rais wa Bashar al-Assad ametoa hakikisho hilo katika mazungumzo yake kwa njia ya simu na rais Vladimir Putin na kukubaliana kuwa makubaliano hayo ni mwongozo muhimu katika kufikia mwafaka wa mgogoro wa Syria.

Rais wa zamani wa Burkina Faso amepewa uraia Cote D'Ivoire

Rais wa zamani wa Burkina Faso Blaise Compaore amepewa uraia wa nchi ya Cote D'Ivoire baada ya maombi yake kukubaliwa na serikali ya nchi hiyo kufuatia kukimbia nchini mwake mwezi Oktoba 2014.

Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari vya taifa, Blaise Compaore pamoja na mdogo wake aliyetajwa kwa jina la Francois wamepewa uraia wa taifa hilo baada ya hatua hiyo kuwa imetangazwa katika katika gazeti la serikali mwezi uliopita.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS