Home » Node

Mhe. Mbarawa ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mbarawa ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), Mhandisi Marcellin Benedict Magesa kuanzia Februari 18 mwaka huu.

Profesa Mbarawa amechukua hatua hiyo kutokana na kuwepo kwa sababu mbalimbali zikiwemo, kushindwa kusimamia matengenezo ya magari na mitambo ya Serikali nchini, kushindwa kusimamia uendeshaji wa matenegenzo ya vivuko vya Serikali nchini pamoja na kushindwa kusimamia ukusanyaji wa mapato kupitia vyanzo mbalimbali.

Haben Girma ni msichana kiziwi na kipofu wa kwanza kuhitimu Havard Law School

Haben Girma ni msichana mwenye miaka 27, kiziwi na kipofu wa kwanza kuhitimu katika shule ya Law (Havard Law School) huko marekani, Haben anagombania haki za watu vipofu na viziwi duniani. Leo hii Haben Girma ni wakili anayepigania haki za watu walemavu. Haben anasema kuwa yeye ni ushahidi kuwa ukiamini unaweza kufanya kitu basi utaweza kukikamilisha.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS