Home » Node

NRM kwa mara nyingine kimejizolea wingi wa viti Bungeni

Chama tawala nchini Uganda cha Rais Yoweri Kaguta Museveni, NRM kwa mara nyingine kimejizolea wingi wa viti Bungeni katika uchaguzi wa Rais na Wabunge uliofanyika juma lililopita nchini humo.

Kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi yanayoendelea kutolewa na Tume ya Uchaguzi ya Uganda cha NRM kinatarajiwa kuchukua viti 427 vya ubunge wakati matokeo ya mwisho yatakapokuwa yametollewa wiki ijayo.

WAZIRI MKUU Kasim Majaliwa amekutana na mabalozi wa Uturuki, Ireland na Uswisi

WAZIRI MKUU Kasim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na mabalozi watatu kutoka nchi za Uturuki, Ireland na Uswisi pamoja na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa hapa nchini.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na mabalozi hao leo (Jumanne, Februari 23, 2016), ofisini kwake, Magogoni jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu aliwashukuru mabalozi hao kwa kuja kujitambulisha rasmi na kwa pongezi walizokuja kumpatia na kuahidi ushirikiano zaidi pamoja na nchi hizo.

Rais Magufuli akutana na Mjumbe Maalum wa Nkurunziza

Rais wa Jamhuri ya Burundi Mheshimiwa Pierre Nkurunziza amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuwa hali ya Burundi ni shwari na kwamba tangu jana (Februari 22, 2016) nchi hiyo imepokea ugeni mkubwa wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mheshimiwa Ban Ki-moon na inatarajia kupokea marais watano kutoka nchi za Umoja wa Afrika tarehe 25 Februari, 2016.

Ugiriki kutumia kidiplomasia kutstua tatizowahamiaji na wakimbizi

Serikali ya Ugiriki imesema imeanza juhudi za kidiplomasia kutatua tatizo la maelfu ya wahamiaji na wakimbizi waliozuiliwa katika eneo la mpaka na Macedonia tangu pale nchi hiyo iliponaza kuwazuia wakimbizi kutoka Afghanistan.

Zaidi ya wahamiaji elfu tano wanazuiliwa tangu Jumapili katika eneo la Idomeni mji wa mwisho wa Ugiriki kabla ya kuingia nchini Macedonia ambapo shughuli za zimepungua kuligana na duru za polisi.

Polisi nchini Indonesia imekamata meli 27

Polisi nchini Indonesia imekamata meli 27 za kigeni zilizokuwa zikifanya uvuvi haramu, katika hatuwa ya kupambana na Uvuvi haramu. Miongoni mwa meli zilizokamatwa ni pamoja na meli kutoka Ufilipino, Vietnam, Malaisia na Myanamar.

waziri anaehusika na maswala ya Uvuvi nchini Indonesia Susi Pudjiastuti amesema meli hizio zilikamatwa zote zikifanya uvuvi kinyume cha sheria katika eneo la indonesia, huku meli nyingine nne za Indonesia zikikamatwa kwa kufanya shughuli za uvuvi bila kibali.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS