NRM kwa mara nyingine kimejizolea wingi wa viti Bungeni
Chama tawala nchini Uganda cha Rais Yoweri Kaguta Museveni, NRM kwa mara nyingine kimejizolea wingi wa viti Bungeni katika uchaguzi wa Rais na Wabunge uliofanyika juma lililopita nchini humo.
Kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi yanayoendelea kutolewa na Tume ya Uchaguzi ya Uganda cha NRM kinatarajiwa kuchukua viti 427 vya ubunge wakati matokeo ya mwisho yatakapokuwa yametollewa wiki ijayo.






















