Home » Node

Nilikosea, Olduvai Gorge iko Tanzania, Bi Odinga

Mwanawe aliyekuwa waziri mkuu wa Kenya, Raila Odinga, Rosemary, amekiri kuwa alikosea alipodai kuwa bonde la Olduvai Gorge liko Kenya ilhali liko Tanzania.

''Bonde la Oldupai ama Olduvai liko Tanzania, nimekubali kuwa nilikosea nilipokuwa nikihutubia mkutano wa viongozi wa vijana kutoka kote duniani nikiwa New York Marekani(International Young Leaders Assembly).

''Nahisi kama ambaye nimewakosea ndugu zangu kutoka Tanzania''.

Bomba kubwa la kusambazia Maji kutoka chanzo cha Maji cha Ruvu Chini waelekea kamilika

Huduma ya Usambazaji wa Maji Safi katika jiji la Dar es salaam inatarajiwa kuimarika kwa kuwafikia wananchi wengi zaidi. Ujenzi wa Bomba kubwa la kusambazia Maji kutoka chanzo cha Maji cha Ruvu Chini, Bagamoyo mkoani Pwani.

Mradi huo unajengwa na Kampuni ya JBG Gauff Ingenieure kwa gharama ya shilingi Bilioni 141 ambazo zimetolewa na Serikali ya Tanzania na una  jumla ya urefu wa kilometa 55.9.

Waziri mkuu Kasim Majaliwa amemsimamisha kazi daktar Mtwara

Waziri mkuu Kasimu Majaliwa amemsimamisha kazi daktari mmoja wa  hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mtwara, Ligula baada ya kufuatia tuhuma za kumuomba mgonjwa  rushwa ya shilingi laki moja na kumuandikia dawa ambazo hazijatumika.

Aidha ya dawa yaliyopo karibu na hospitali hiyo kufungwa mara moja baada yeye kuondoka katika eneo la hospitali kutokana na madaktari kujihusisha na biashara na kuacha kutumia dawa za serikali zilizopo katika hospitali hiyo.

Bao la kwanza la Samatta akiichezea KRC Genk

KRC Genk imefanikiwa kuifunga Club Brugge mabao 3-2, lakini story kubwa ni kumshuhudia Mbwana Ally Samatta akifunga bao la tatu ambalo lilikuwa ni bao lake la kwanza tangu ajiunge na timu hiyo.

Ulikuwa ni mchezo wake wa nne akitokea benchi leo kwenye mchezo ambao Genk walikuwa wakihitaji pointi tatu muhimu huku wakihitaji kumaliza katika nafasi 6 za juu ili waweze kuingia kwenye play off. wamefanikiwa kupata ushindi huo  na kutengeneza mazingira mazuri ya kuweza kumaliza katika nafasi 6 za juu kwenye ligi.

KESI YA MWANASIASA WA RWANDA INGABIRE YATUA MAHAKAMA YA AFRIKA

Kesi ya mwanasiasa mfungwa raia wa Rwanda,Bibi  Victoire ingabire (42), itasikilizwa katika mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (AfCHPR) yenye makao yake makuu jijini Arusha Ijumaa, Machi 4 2016.

Ingabire analalamika kuvunjiwa haki zake za msingi za binadamu na haki katika mchakato wa usikilizishwaji kesi yake nchini Rwanda kama ilivyoainishwa katika mkataba wa Afrika na haki za binadamu chini ya vifungu 1,3,5,7,10,11,28 and 19.

Mkutano wa 17 wa kawaida wa wakuu wa nchi zaJumuiya ya Afrika Mashariki

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasili Mkoani Arusha ambako pamoja na mambo mengine ataongoza Mkutano wa 17 wa kawaida wa wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika Jumatano tarehe 02 Machi, 2016 Mjini Arusha.

Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) Rais Magufuli amelakiwa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na serikali pamoja na vikundi vya burudani za ngoma kabla ya kuelekea Arusha Mjini.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea misaada ya wakazi wa vijiji vya Mtondo na Nanjaru

WAZIRI APOKEA MISAADA KWA WALIOPATWA NA MAAFA RUANGWA

 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea misaada mbalimbali kwa ajili ya wakazi wa vijiji vya Mtondo na Nanjaru wilayani Ruangwa mkoani Lindi ambao nyumba zao ziliezuliwa na upepo Januari mwaka huu.

Akizungumza na wananchi wa vijiji hivyo  (Jumapili, Februari 28, 2016), Waziri Mkuu alisema maafa huwa yanakuja bila kutarajiwa na akatumia fursa hiyo kuwashukuru wadau waliotoa misaada ya chakula, magodoro, mashuka, vitenge, mabati na mbegu za mazao.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS