Home » Node

Polisi wasema walimpeleka Besigye Nyumabani kwake

Msemaji wa chama cha Forum for Democratic Change Ssemujju Ibrahim Nganda amethibitisha kwamba mgombea urais wa chama hicho Dkt Kizza Besigye aliyekuwa amekamatwa na polisi sasa ameachiliwa huru.

Kanali huyo mstaafu ambaye ni kigogo wa upinzani nchini Uganda alikuwa amekamatwa katika kitongoji cha Naguru, mjini Kampala katika nyumba ambayo upinzani ulidai wizi wa kura ulikuwa ukifanyika.

Wafuasi wa upinzani, wakiambatana na kanali Besigye, wanadai walifumania watu wakiiba kura na wakataka usaidizi wa polisi kukagua nyumba hiyo lakini wakazuiliwa.

Matokeo ya Uchaguzi mkuu nchini Uganda yaanza kutolewa

Uchaguzi mkuu nchini Uganda unafanyika leo, wengi wakiangazia sana uchaguzi wa urais ambapo kuna jumla ya wagombea wanane.

Mwanamke ni mmoja, Maureen Kyalya.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahidi kwamba matokeo yatakuwa tayari katika kipindi cha saa 48 baada ya kufungwa kwa vituo saa kumi alasiri.

Baada ya hapo, tume inatarajia kuwa ikitangaza matokeo ya urais baada ya kila saa mbili.

Kansela kuguswa na hali ya kibinadamu inayoshuhudiwa nchini Syria

Kansela wa ujerumani Angela Merkel ameeleza kuguswa na hali ya kibinadamu inayoshuhudiwa nchini Syria na kudai kuwa haivumiliki na kurelejea wito wake wa kupiga marufuku ndege za kivita kuruka maeneo ya raia.

Kiongozi huyo ameongeza kuwa mashambulizi ya anga yanayoungwa mkono na Urusi mjini Alepo yamesababisha wakazi wengi kukimbia kaskazini mwa syria.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS