Home » Node

Rais Dr. Magufuli amlilia Mhe. Aboud Jumbe Mwinyi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na pia Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Aboud Jumbe Mwinyi kilichotokea leo tarehe 14 Agosti, 2016 Jijini Dar es Salaam.

NIDA yashinda Tuzo Nane Nane

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA imeibuka Mshindi wa Kwanza kati ya Taasisi na Wizara za Serikali zinazotoa huduma kwa Jamii, wakifuatiwa na Wizara ya Maji na Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali wakichukua Nafasi ya Tatu katika Maonyesho ya 23 ya Sikukuu ya Wakulima Nananane yaliyofanyika Mjini Lindi Kuanzia Tarehe 01 Agosti 2016 hadi Tarehe 10 Agosti 2016 katika Viwanja vya Ngongo wilaya ya Lindi Mjini.

Rais Dr. Magufuli Ameweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Daraja la waenda kwa miguu la Furahisha

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli pamoja na Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Edwin Ngonyani, Mbunge wa Sumve Richard Ndassa wakipiga makofi mara baada ya tukio la uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Daraja la waenda kwa miguu la Furahisha pamoja na Upanuzi wa barabara ya Mwanza-airport.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS