Home » Node

Awamu ya pili ya mazungumzo ya amani kuhusu mzozo wa Burundi Kuanza tena

Awamu ya pili ya mazungumzo ya amani kuhusu mzozo wa Burundi, yamepangwa kurejelewa kuanza siku ya jumamosi tarehe 9 mwezi huu wa julai hadi Julai 12 mjini Arusha nchini Tanzania, lakini bila ya kushirikishwa kwa wanasiasa wa muungano wa upinzani CNARED.

Taarifa hii imechapishwa kupitia mtandao wa twitter wake Macocha Tembele, mkurugenzi wa ofisi ya mratibu wa mazungumzo hayo, rais wa zamani wa Tanzania Benjamin Mkapa.

NIDA ya kwanza katika Maadhimisho ya Maonyesho ya 40 ya Kibiashara Kimataifa

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa imeibuka Mshindi wa kwanza katika Maadhimisho ya Maonyesho ya 40 ya Kibiashara Kimataifa – Sabasaba kama Banda Bora katika Kutoa Huduma Bora na yenye Viwango kwa Umma inayotoa mchango katika Kuwezesha Kuunganisha Biashara na Masoko pamoja na Uwekezaji (Best Exhibitor Trade and Investment Support Dar Es Salaam International Trade Fair – DITF) yaliyoanza tarehe 28/06/2016 – 08/06/2016

Rais Kagame akiwa na mwenyeji wake Rais Magufuli, amefungua rasmi maonesho ya 40 ya kimataifa ya Biashara

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewahakikishia wafanyabiashara wa Rwanda kuwa bandari ya Dar es salaam ni salama kwa wao kupitisha mizigo na ameahidi kuwa Serikali ya Tanzania inaendelea kuchukua hatua za kuiboresha bandari hiyo na kurahisisha biashara kati ya nchi hizi mbili.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 25 Juni, 2016 amezindua kituo cha mawasiliano cha Jeshi la Polisi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 25 Juni, 2016 amezindua kituo cha mawasiliano cha Jeshi la Polisi ambacho kitarahisisha utoaji wa taarifa za uhalifu na kuharakisha askari polisi kufika katika eneo la tukio.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS