Home » Node

Kiongozi FDLR amejiondoa katika kundi

Kiongozi wa ulinzi wa karibu na mkuu wa waasi wa kihutu wa Rwanda waliopo nchini DRCongo wa FDLR amejiondoa katika kundi hilo na kujisalimisha nchini Rwanda, duru rasmi kutoka Kigali zimethibitisha.

Kaptaine Aphrodice Nyirimpeta aliwasili Kigali Feb 12 na kupelekwa Mutobo kaskazini mwa nchi hiyo, kambi inayowapokea wapiganaji zamani na kuwapiga msasa kabla ya kujiunga na jamii.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi yakanusha taarifa ya Kuanza mchakato Kura ya Maoni

Katika taarifa iliyotolewa  na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo imesainiwa na mkurugenzi wa Uchaguzi Ndg KAilima Ramadhani, inaeleza kwamba taarifa iliyotolewa na Gazeti la Nipashe toleo Na:0578761 la tarehe 16 Februari 2016 kwamba "MCHAKATO WA KURA YA MAONI YA KATIBA INAYOPENDEKEZWA UMEIVA" kwamba taarifa hizi SIO ZA KWELI NA ZINALENGA KUUPOSHOSHA UMMA WA WATANZANIA.

Mawakili wa Victoire Ingabire kupata ugumu wakati wanapotaka kuonana na mteja wao

Mawakili wa kiongozi wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire anayetumikia kifungo cha miaka 15 jela, wamelalamika kupata ugumu wakati wanapotaka kuonana na mteja wao wakati huu wakiandaa kesi ya kupitiwa upya kwa hukumu yake katika mahakama ya Afrika.

 

Wakili wa Ingabire, Gatera Gashabana, amesema February 5 mwaka huu alienda kuonana na mteja wake kwa maandalizi ya kuanza kusikilizwa kwa kesi yake katika mahakama ya haki za binadamu mjini Arusha Tanzania, lakini hakuweza kukutana nae baada ya kuzuiwa na maofisa wa gereza.

Wataalamu: Biashara ya meno ya Tembo haiwezi kumalizwa hivi karibuni

Wataalamu wa mazingira wanasema kuwa biashara ya meno ya Tembo haiwezi kumalizwa hivi karibuni kwakuwa kwa sehemu kubwa wanaofanya biashara hiyo ni watu wenye ushawishi kwenye Serikali.

 

Akizungumza kwenye mjadala wa shirikisho la Marekani linalofanya utafiti wa kisayansi kuhusu wanyamapori, profesa wa bailojia katika chuo kikuu cha Washington, Samuel Wasser, amesema biashara hii inaongozwa na watu wachache wenye fedha na ushawishi mkubwa kwenye Serikali.

 

Umoja wa Mataifa unachunguza Afrika ya Kati

Umoja wa Mataifa unachunguza tuhuma mpya za vitendo vya udhalilishaji wa kingono vinavyofanywa na askari wake wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, tuhuma ambazo zitakuwa si za kwanza kuelekezwa kwa wanajeshi hao.

 

Msemaji wa umoja wa Mataifa, Farhan Haq, amesema kuwa tayari timu ya wachunguzi kutoka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, imeshatumwa nchini humo kuchunguza tuhuma hizi mpya dhidi ya walinda amani wake.

 

Cameroon vimetekeleza mashambulizi Boko Haram nchini Nigeria,

Vikosi vya Serikali ya Cameroon vimetekeleza mashambulizi kulenga kambi muhimu za wapiganaji wa kundi la Boko Haram nchini Nigeria, huku ikiripotiwa kuuawa kwa wapiganaji wengi wa kundi hilo pamoja na kukamata zana za kivita zilizokuwa zinatumiwa na wapiganaji hao.

 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na jeshi la Cameroon imesema kuwa operesheni dhidi ya wapiganaji wa Boko Haram, ilitekelezwa juma moja lililopita kwenye eneo la Ngoshe, eneo la mpaka wa nchi hiyo na Nigeria.

 

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS