Kiongozi FDLR amejiondoa katika kundi
Kiongozi wa ulinzi wa karibu na mkuu wa waasi wa kihutu wa Rwanda waliopo nchini DRCongo wa FDLR amejiondoa katika kundi hilo na kujisalimisha nchini Rwanda, duru rasmi kutoka Kigali zimethibitisha.

Kaptaine Aphrodice Nyirimpeta aliwasili Kigali Feb 12 na kupelekwa Mutobo kaskazini mwa nchi hiyo, kambi inayowapokea wapiganaji zamani na kuwapiga msasa kabla ya kujiunga na jamii.























