Home » Node

Rais Dkt. Magufuli afanya uteuzi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Modestus Francis Kipilimba kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA). Kabla ya Uteuzi huu Dkt. Kipilimba alikuwa Mkurugenzi wa Menejimenti ya Udhibiti (Director of Risk Management) katika Benki Kuu ya Tanzania. Dkt. Kipilimba anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Dikson Maimu ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Uteuzi huo utaanza tarehe 15 Februari, 2016

Mamlaka Ya Vitambulisho Vya Taifa (NIDA)

UMUHIMU WA KITAMBULISHO

Vitambulisho vya Taifa ni chachu ya maendeleo ya Kiuchumi, kijamii na  kiusalama

1. Vitasaidia kuongeza wigo wa mapato ya Serikali

2. Vitasaidia kumtambua mhusika kirahisi anapohitaji kupatiwa huduma katika taasisi mbalimbali kama vile benki, taasisi za mikopo na huduma za afya.

3. Vitarahisisha kuwatambua wakwepaji wa kurejesha mikopo kutoka kwenye benki na asasi mbalimbali za fedha nchini.

Umoja wa Mataifa wasisitiza haja ya kutimiza ahadi

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw Ban Ki-moon amesema ahadi ya azimio la Umoja huo kwa watu walio kwenye hali duni inapaswa kuendelea kutimizwa.

Katibu huyo amesema mwaka wa 2015 ulikuwa ni mwaka wa migogoro, na kutolea mifano ya Syria ma Yemen. Alisema matukio kama hayo ambayo yanakiuka haki za kimsingi za kibinadamu ni kinyume na maazimio ya Umoja huo na ni changamoto kwa baraza la usalama kutimiza wajibu wake.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS