Ukaguzi wa Taarifa za Biashara
Maboresho katika Mfumo wa Mashine za EFD
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), inapenda kuwafahamisha wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla kwamba inaboresha mfumo wa mashine za kielektroniki za kodi (EFD). Ili maboresho hayo yapokelewe na kukubalika katika mashine za EFD, wafanyabiashara wanashauriwa kuzima na kuwasha mashine za EFD.
IGP awaapisha makamishina wapya
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo, Wakurugenzi watatu Wasitishiwa mikataba.
Na JacquilineMrisho MAELEZO
Fahamu faida za tikitimaji
#333333; font-family:helvetica,arial,lucida grande,tahoma,verdana,arial,sans-serif; font-size:14px">Licha ya 92% ya tikiti maji kuwa ni maji, bado zile 8% zilizobaki zina faida kubwa sana kiafya jambo linaloonekana kutofahamika kwa wengi.
Rais Dkt. Magufuli afanya uteuzi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Modestus Francis Kipilimba kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA). Kabla ya Uteuzi huu Dkt. Kipilimba alikuwa Mkurugenzi wa Menejimenti ya Udhibiti (Director of Risk Management) katika Benki Kuu ya Tanzania. Dkt. Kipilimba anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Dikson Maimu ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Uteuzi huo utaanza tarehe 15 Februari, 2016
Mamlaka Ya Vitambulisho Vya Taifa (NIDA)
UMUHIMU WA KITAMBULISHO
Vitambulisho vya Taifa ni chachu ya maendeleo ya Kiuchumi, kijamii na kiusalama
1. Vitasaidia kuongeza wigo wa mapato ya Serikali
2. Vitasaidia kumtambua mhusika kirahisi anapohitaji kupatiwa huduma katika taasisi mbalimbali kama vile benki, taasisi za mikopo na huduma za afya.
3. Vitarahisisha kuwatambua wakwepaji wa kurejesha mikopo kutoka kwenye benki na asasi mbalimbali za fedha nchini.
TRA yataka elimu ya ulipaji kodi itolewe shuleni
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari nchini wakiandaliwa vizuri kwa kuwapati elimu ya kodi, taifa litapata walipakodi walio waadilifu.
Umoja wa Mataifa wasisitiza haja ya kutimiza ahadi
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw Ban Ki-moon amesema ahadi ya azimio la Umoja huo kwa watu walio kwenye hali duni inapaswa kuendelea kutimizwa.
Katibu huyo amesema mwaka wa 2015 ulikuwa ni mwaka wa migogoro, na kutolea mifano ya Syria ma Yemen. Alisema matukio kama hayo ambayo yanakiuka haki za kimsingi za kibinadamu ni kinyume na maazimio ya Umoja huo na ni changamoto kwa baraza la usalama kutimiza wajibu wake.
















