Home » Node

Wakuu wa mikoa na wilaya watakiwa kutoa taarifa ya upungufu wa vitanda hospitalini

Waziri wa maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto UMMY MWALIMU, amewaagiza wakuu wa mikoa na wilaya kote nchini kutoa taarifa ya upungufu wa vitanda katika hospitali za serikali zilizopo katika maeneo yao ili serikali iendelee kuboresha huduma za afya

Waziri MWALIMU ametoa aagizo hilo katika hospitali ya Taifa Muhimbili jijini DSM, wakati kipokea vitanda na magodoro vyenye thamani ya Shilingi Milioni 88.7 kwa ajili ya wodi mpya ya wazazi kufuatia agizo la Rais Dkt. JOHN MAGUFULI.

Polisi nchini Indonesia imewakamata zaidi ya watu 30

Polisi nchini Indonesia imewakamata zaidi ya watu 30 kutoka makundi ya kijihadi wanaoshukiwa kupanga mashambulizi ya kigaidi nchini humo.

Kukamatwa huko kunakuja baada ya taarifa za kinteljensia kuonesha kuwa, washukiwa hao walikuwa wanapanga kutekeleza mashambulizi ya kigaidi katika uwanja wa ndege katika siku zijazo.

Aidha, polisi wanasema watu hao wamekamatwa baada ya kuanza kwa operesheni ya kuwatafuta magaidi baada ya kutokea kwa shambulizi ya bomu mjini Jakarta na kusababisha vifo vya watu wanne na wenhine kujeruhiwa mwezi uliopita.

Uturuki haitaruhusu mpaka wa syria wa mjini Azaz kuangukia mikononi mwa wapiganaji

Uturuki imesema haitaruhusu mpaka wa syria wa mjini Azaz kuangukia mikononi mwa wapiganaji wa kikurdi wa nchini syria na kutoa onyo la makabiliano mara moja ikiwa watasonga mbele kukaribia eneo hilo.

Waziri mkuu wa uturuki Ahmet Davutoglu amekaririwa akizungumza hayo katika kituo cha televisheni cha NTV.

Uturuki imeshambulia ikiwalenga wapiganaji wa kikurdi wa syria tangu wikiendi huku ankara ikisisistiza ilikuwa ikijibu mashambulizi.

Kitengo cha intelijensia Drc kimemuachilia huru Martin Fayulu

Kitengo cha intelijensia ya jeshi nhcini Drc kimemuachilia huru kiongozi wa chama cha siasa cha upinzani Martin Fayulu, baada ya kumkamata mapema Jumapili kwenye makao makuu ya chama chake mjini Kinshasa.

Kiongozi wa chama cha ECIDE, akiwa pia mjumbe wa muungano wavyama vya upinzani na mgombea urais, Martin Fayulu aliwatolewa wito wafuasi wake kususia shughuli mbalimbali Februari 16 akidai uchaguzi ufanyike ndani ya muda uliopangwa kikatiba, kuheshimu Katiba na kanuni za kupishana madarakani kidemokrasia.

Polisi nchini Uganda wamelazimika kutumia mabomu

Polisi nchini Uganda wamelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa Mgombea urais wa chama cha upinzani cha FDC nchini Uganda Kizza Besigye ambaye alikamatwa na kuzuiliwa kwa muda na maafisa wa polisi mjini Kampala.

Kwa mujibu wa AFP Besigye,ambaye kwa mara tatu mfululizo ameangushwa katika uchaguzi na raisi museven alikamatwa na polisi baada ya kufanya kampeni zake mjini kampala huku msafara wake ukisindikizwa na mamia ya wafuasi, ndipo walipotumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi hao na kukamkamata mwanasiasa huyo.

Zoezi la kuhesabu kura linaendelea nchini jamuhuri ya afrika ya kati

Zoezi la kuhesabu kura linaendelea nchini jamuhuri ya afrika ya kati baada ya kukamilika kwa upigaji kura siku ya jumapili katika uchaguzi wa duru la pili ambao unatazamiwa huenda ukatamatisha uhasama na ghasia za kidini katika taifa hilo.

Kura zilipigwa chini ya ulinzi mkali huku waangalizi wa umoja wa mataifa wakisambazwa nchi nzima na kushuhudia uchaguzi ukitamatika kwa amani.

Zoezi hilo la kuhesabu kura lilianza jana jumapili katika madarasa ya shule zilizotengwa kuwa vituo vya kupigia kura nchini humo.

Rais Dkt Magufuli amewateua mabalozi watatu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa mabalozi watatu katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa.

Rais Magufuli pia amefanya uteuzi wa makamishna wanne wa Jeshi la Polisi na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, imewataja mabalozi walioteuliwa kuwa ni Dkt. Asha-Rose Mtengeti Migiro, Mheshimiwa Mathias Meinrad Chikawe na Dkt. Ramadhan Dau.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS