Home » Node

Waziri mkuu Matteo Renzi ameionya nchi ya Misri

Wakati Serikali ya Italia ikimzika raia wake Giulio Regeni, waziri mkuu Matteo Renzi ameionya nchi ya Misri na kusema kuwa urafiki wao uko mashakani kutokana na uchunguzi wao kushindwa kueleza ni namna gani raia wake aliuawa.

Waziri mkuu Renzi amesema Serikali ya Misri ilitoa ushirikiano kwenye madai yake kwamba wachunguzi wa nchi yake wahusishwe kufanya uchunguzu kuhusu kifo cha Regen ambaye mwili wake ulipatikana ukiwa na majeraha yanayoenesha ishara kuwa aliteswa kabla ya kuuawa.

Watungua 'chopa' wanne wafungwa miaka 60

Raia wanne wa Tanzania waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya mauji ya mwanamazingira raia wa Unigereza ambaye helcopter yake ilidunguliwa, wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la kumiliki silaha za moto kinyume cha sheria.

Licha ya watuhumiwa hao kutokiri kuhusika na mauji ya rubani huyo, iwapo watapatikana na hatia ya kosa la kuu, huenda wakahukumiwa kunyongwa kwa mujibu wa sheria za Tanzania, ambapo hata hivyo haijatekeleza kwa muda mrefu adhabu hiyo.

Roboti ya Mende kuokoa wahanga wa maporomoko

Wanasayansi nchini Marekani wametengeneza roboti inayofanana na mende ambayo inaweza kutumiwa kuwaokoa watu kunapotokea tetemeko la ardhi.

Watafiti wanasema roboti hiyo inatumia mbinu zinazotumiwa na mende kutembea kwenye nyufa kupenya vifusi na kuwaokoa walionaswa katika maporomoko.

Wanasayansi hao wanasema kuwa endapo roboti hiyo inawezavishwa kamera kisha ikatumwa kwenye vifusi vya jengo lililoporomoka inaweza kurahisisha uchunguzi wa usalama wa vifusi kabla ya makundi waokoaji kuingia.

Ukubwa wa roboti hiyo ni sawa na kiganja cha mwanadamu.

Aliyeishi muda mrefu na moyo wa kupandikizwa afariki

Bw McCafferty alipatikana na maradhi ya moyo akiwa na umri wa miaka 39.

Alifanyiwa upasuaji na Sir Magdi Yacoub.

Upasuaji wa kwanza wa kupandikiza moyo uliofanikiwa ulifanyiwa nchini Afrika Kusini mwaka 1967 na Prof Christiaan Neethling Barnard na kundi la matabibu 30 katika hospitali ya Groote Schuur, Cape Town.

Mgonjwa wao, Louis Washkansky, alifariki siku 18 baada ya kupokea moyo mpya.

Mwanamume aliyeishi muda mrefu duniani na moyo wa kupandikizwa amefariki, baada ya kuishi miaka 33 na moyo huo.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS