Home » Node

Magaidi kuvuliwa uraia, yapitishwa na bunge la Ufaransa

Baraza la chini la bunge la Ufaransa limepitisha mswada wa marekebisho ya katiba yanayolenga kuwavua magaidi uraia wa Ufaransa.

Kwa mujibu wa mswada huo, adhabu hiyo ya ziada itatolewa kwa magaidi au wahalifu wanaokiuka maslahi ya kimsingi ya taifa.

Mtu anayechukuliwa hatua hiyo atanyang'anywa haki zote za kiraia zikiwemo haki ya kuchagua, kuchaguliwa na kufanya kazi kama mtumishi wa serikali.

Watu 15 wafariki baada ya gari lililobebea gesi kulipuka nchini Pakistan

Takriban watu 15 wakiwemo watoto 10 wa shule wamefariki na wengine wengi kujeruhiwa, kufuatia gari la kubebea gesi kulipuka leo asubuhi baada ya kugongana na gari jingine mashariki mwa Pakistan.

Ajali hiyo ilisababisha moto mkubwa, uliofunika gari mbili zilizokuwa zikipita pamoja na riksho mbili zilizokuwa zikibeba watoto wanaokwenda shule. Majeruhi wakiwemo wanawake na watoto wa shule wamepelekwa hospitali, na baadhi yao wako katika hali mahututi.

Tanzania Kuanzisha kitengo cha uhalifu wa wanyama pori kupambana na ujangili

Waziri wa Mali asili na Utalii wa Tanzania Profesa Jumanne Maghembe amesema Tanzania imepanga kuanzisha Kitengo maalumu cha kukabiliana na uhalifu wa Wanyamapori ikiwa kwenye juhudi ya kuzidisha mapambano yake dhidi ya ujangili.

Hatua hiyo imekuja siku chache tu tangu majangili waitungue helikopta iliyokuwa kwenye doria ya kawaida katika Hifadhi ya Maswa iliyopo kusini mwa Mbuga ya Taifa ya Serengeti, na kumuua rubani ambaye ni Muingereza Roger Gower. Katika tukio hilo hadi sasa wameshakamatwa watu tisa.

Treni zaua watu takribani tisa na kujeruhi zaidi ya 100 ujerumani

Treni Mbili za abiria zimegongana uso kwa uso kusini mwa Ujerumani leo Jumanne, na kuua watu takribani tisa na kujeruhi zaidi ya 100, katika moja ya ajali mbaya ya treni kushuhudiwa katika nchi hiyo miaka ya karibuni.

Mamia ya waokoaji wameendelea kuwaokoa abiria zaidi walionaswa katika mabaki ta treni hiuzo  katika eneo la msitu karibu na Bad Aibling,mji ulio umbali wa kilomita 60 Kusini Mashariki mwa Munich.

Mkuu wa zamani wa jeshi la Kongo kuwania nafasi ya urais katika uchaguzi wa Machi 20

Mkuu wa zamani wa jeshi la Kongo na mshauri wa rais ametangaza  mpango wa kuwania nafasi ya urais katika uchaguzi wa Machi 20 kukabiliana na Rais wa sasa Denis Sassou Nguesso, ambaye amekuwa madarakani nchini Congo-Brazzaville kwa zaidi ya miaka 30.

Jenerali  Jean-Marie Michel Mokoko ameiambia AFPkwa njia ya simu akiwa mjini Bangui kuwa anajisikia kuitwa kuwatumikia wananchi na ameamua kuingia ulingoni kugombea.

Huko nchini Kenya mcheza kamari raia wa Tanzania ameuawa

Huko nchini Kenya mcheza kamari raia wa Tanzania ameuawa na kundi la watu kwa kupigwa mawe,baada ya kuwaua watu wawili kufuatia kupoteza pesa zake katika mchezo huo na kushindwa kukubaliana na hali hiyo, polisi wamesema leo Jumanne.

Mtanzania huyo  alipandwa na  hasira baada ya kupoteza dola 300 katika casino moja wilayani  Eastleigh mjini Nairobi  majira ya asubuhi leo  Jumanne, na kumshambulia meneja wa casino baada ya kukataa kumkopesha fedha ili aendelee kucheza.

(ICC) ishughulikie manung’uniko ya kuwawajibisha viongozi wa Afrika pekee

Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa kivita  (ICC) imetakiwa kushughulikia manung’uniko yanayohusu kuwawajibisha viongozi wa Afrika pekee ili kukifanya chombo hicho kiendelee kutoa haki na kuheshimika

Akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na mahakama hiyo katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa jijini Arusha nchini Tanzania, Waziri wa Katiba na Sheria  nchini Tanzania Dr.Harisson Mwakyembe  ameitaka mahakama hiyo kufanyia kazi manung`uniko ya bara la Afrika licha ya Tanzania kuunga mkono shughuli za mahakama hiyo lakini bado iko kwenye msimamo wa nchi hizo.

Jocelyn Elliot, mwanamke raia wa Australia aliyetekwa nyara

Jocelyn Elliot, mwanamke raia wa Australia mwenye umri wa miaka themanini aliyetekwa nyara na wanajihadi nchini Burkina Faso akiwa na mume wake amesema  siku ya jumatatu kuwa ana matumaini ya kukutana na mume wake Ken hivi karibuni kuendeleza shughuli zao , lama ilivyokuwa hapo awali.

Elliott ameyasema hayo punde baada ya kupokelewa na rais wa nchi hiyo Christian Kabore  ambaye amesema kusikitishwa na kitendo cha kutekwa kwa raia hao wa Australia.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS