Magaidi kuvuliwa uraia, yapitishwa na bunge la Ufaransa
Baraza la chini la bunge la Ufaransa limepitisha mswada wa marekebisho ya katiba yanayolenga kuwavua magaidi uraia wa Ufaransa.
Kwa mujibu wa mswada huo, adhabu hiyo ya ziada itatolewa kwa magaidi au wahalifu wanaokiuka maslahi ya kimsingi ya taifa.
Mtu anayechukuliwa hatua hiyo atanyang'anywa haki zote za kiraia zikiwemo haki ya kuchagua, kuchaguliwa na kufanya kazi kama mtumishi wa serikali.


























