Home » Node

Jaji wa mahakama ya juu Kenya apatikana na hatia

Jaji mmoja wa Mahakama ya Juu nchini Kenya Phillip Tunoi amepatikana na hatia ya kukiuka maadili ya kazi baada ya uchunguzi uliofanywa na kamati iliyoundwa na Tume ya Huduma za Mahakama.

Jaji Tunoi amepatikana na hatia ya "kujihusisha kwa njia isiyofaa" na mtu ambaye alikuwa akimwakilisha mhusika katika kesi ya uchaguzi, jambo amablo ni ukiukaji wa maadili.

Jaji Mkuu Willy Mutunga amempendekezea Rais Uhuru Kenyatta aunde jopo maalum kwa mujibu wa Katiba.

Jopo hilo litakuwa na jukumu la kuchunguza kikamilifu madai yaliyotolewa dhidi ya Jaji Tonui.

BASATA wametoa ujumbe kuwataka LINO na kurudi mezani

Baraza la sanaa Tanzania (BASATA) limefungua makucha na kuitaka kampuni ya LINO waandaaji wa mashindano ya Miss Tanzania kurudi mezani na kamati ya mashindano hayo ambayo ilijitoa wiki kadhaa nyuma kushiriki katika mashindano hayo ambayo awali yalikuwa yamefungiwa.

Basata  wametoa ujumbe kuwataka LINO na kurudi mezani na kuangalia namna bora ya kusonga mbele kwa kuweka mipaka ya utendaji kati yake na kamati hiyo.

Baraza la mawaziri Upinzani hili hapa

Baraza ambalo litakuwa na lengo la kuishinikiza serikali ya Rais Magufuli kutimiza kile alichoahidi kwa Watanzania.

Baraza hilo ni kama ifuatavyo;

BARAZA KIVULI LA MAWAZIRI

Wizara ya Ofisi ya Rais, Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora.

Mawaziri – Jaffar Michael

Naibu Waziri – Joseph Nkundi na Ruth Mollel

Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Waziri – Ali Saleh Abdalla

Naibu Waziri – Pauline Gekul

Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu

Rais Dkt Magufuli azindua Mwaka wa mpya wa siku ya Sheria

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph katika picha ya pamoja na jaji mkuu wa Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman, Waziri wa katiba na sharia Dr. Harson Mwakyembe,Naibu spika wa Bunge Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Tulia Ackson, jaji Mkuu wa Kenya Dkt. Willy Mutunga pamoja naviongozi mbalimbali wa Dini mara baada uzinduzi wa Mwaka Mpya wa Mahakama katika Siku ya Sheria Duniani katika uwanja wa Mahakama mtaa wa Chimala eneo la Ocean Road jijini Dar es salaam February 4, 2016

 

India: Wanafunzi Watanzania wahofia usalama wao

Licha ya serikali ya India kutangaza kuwa watu 5 wamekamatwa kwa kosa la kuwashambulia na kumvua nguo mwanafunzi mmoja raia wa Tanzania, hofu bado imetanda miongoni mwa takriban wanafunzi

150 wa chuo cha Acharya Kaskazini mwa Bangalore .

wawakilishi wa wanafunzi hao wameiambia BBC kuwa uoga na hofu ya kutokea kwa mashambulizi zaidi dhidi yao ndio imewafanya watanzania hao kukataa kutoka makwao wakihofia usalama wao.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS