Home » Node

Serikali yasikitishwa watanzania kudhalilishwa India

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Balozi AUGUSTINE MAHIGA amesema serikali ya TANZANIA imesikitishwa na taarifa za wanafunzi wanne raia wa TANZANIA wanaosoma nchini INDIA kudhalilishwa hivi karibuni wakiwa nchini humo.

 

Akitoa taarifa ya serikali bungeni mjini DODOMA, Waziri MAHIGA amesema serikali imepokea taarifa za wanafunzi hao walio dhalilishwa na kuumizwa kutokana na fujo za kibaguzi zilizotokea BANGALORE nchini INDIA na kumwagiza Balozi wa TANZANIA nchini INDIA kufuatilia suala hilo.

 

AUDIO - Chama kipya cha CM-Tanzania chapata usajili wa muda

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amekisajili chama kipya cha siasa nchini cha Maadili na Uwajibikaji (CM-TANZANIA) na kuwaasa viongozi wake kutekeleza wajibu wao katika kuleta maendeleo ya taifa kwani siasa sio chuki wala uhasama.

Akiongea katika makabidhiano ya cheti cha usajili leo, Jaji Mutungi amevitaka Vyama vya siasa nchini kufanya siasa na sio uanaharakati kwani kwa kufanya hivyo malengo yao yatatimia na kuifanya Tanzania kuwa na amani.

Mawakili wa mashtaka Burundi wamekata rufaa kesi ya jaribio la mapinduzi

Version:1.0 StartHTML:0000000167 EndHTML:0000002672 StartFragment:0000000457 EndFragment:0000002656

Mawakili wa upande wa mashtaka nchini Burundi wamekata rufaa dhidi ya hukumu ya viongozi wa jaribio la mapinduzi wakitaka viongozi hao kupatiwa adhabu ya kifungo cha maisha jela ikiwa ni pamoja na wale saba walioachiwa huru.

 

Mawakili hao Pia walitoa orodha ya majina 34 ya viongozi wa upinzani na wa vyama vya kiraia na waandishi wa habari ambao kwa sasa wapo uhamishoni wakitaka wakabiliwe na mkono wa sheria kwa kuhusika katika jaribio la mapinduzi ya Mei 2015.

Kifaa maalum kinachotumika kuripoti visa

Visa vya dhuluma za kijinsia dhidi ya watoto vimekuwa vikiripotiwa mara kwa mara hasa katika eneo la Pwani ya Kenya, vikidaiwa kuchangiwa na mila za jadi na jamii kutoripoti visa hivyo kwa idara husika, kwa hofu ya unyanyapaa.

 

Shirika moja la kimataifa linalofadhili miradi ya kijamii kuhudumia watoto la Plan international katika jimbo la Kilifi huko Pwani nchini Kenya, limezundua kifaa maalum kinachotumika kuripoti visa hivyo kwa idara husika kupitia simu yenye mtandao wa internate.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS