Serikali yasikitishwa watanzania kudhalilishwa India
Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Balozi AUGUSTINE MAHIGA amesema serikali ya TANZANIA imesikitishwa na taarifa za wanafunzi wanne raia wa TANZANIA wanaosoma nchini INDIA kudhalilishwa hivi karibuni wakiwa nchini humo.
Akitoa taarifa ya serikali bungeni mjini DODOMA, Waziri MAHIGA amesema serikali imepokea taarifa za wanafunzi hao walio dhalilishwa na kuumizwa kutokana na fujo za kibaguzi zilizotokea BANGALORE nchini INDIA na kumwagiza Balozi wa TANZANIA nchini INDIA kufuatilia suala hilo.

















