60% ya mapato ya mifuko ya afya kuboresha huduma za afya
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameagiza asilimia 60 ya mapato yanayopatikana katika mifuko ya afya kutumika kwa ajili ya kuboresha huduma za afya.
Waziri MWALIMU amesema hayo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalumu mkoa wa TABORA, MUNDE TAMBWE aliyetaka kufahamu mpango wa serikali katika kuboresha huduma za afya kwenye mikoa ya Tabora, Katavi na Simiyu.





















