Umoja wa Mataifa umetuma mialiko kwa ajili ya mazungumzo mapya ya amani nchini Syria
Umoja wa Mataifa umetuma mialiko kwa ajili ya mazungumzo mapya ya amani nchini Syria yatakayofanyika mjini Geneva Uswisi juma hili, huku wawakilishi wa upinzani wakijadili kuhusu kuhudhuria au la.
Mialiko imetolewa huku vikosi vya serikali kwa kusaidiwa na ndege za kivita za Urusi vikifanikiwa kuuteka mji wa waasi kusini mwa Syria , katika ushindi wao wa karibuni tangu Moscow ilipoanza kampeni ya mashambulizi ya anga mwezi Septemba mwaka jana.






























