Ijue Benki kuu ya Tanzania
Benki Kuu ya Tanzania ni benki ya kitaifa inayosimamia masuala ya kibenki na kifedha. Makao yake makuu yapo Dar es Salaam nchini Tanzania.
Benki Kuu ya Tanzania ni benki ya kitaifa inayosimamia masuala ya kibenki na kifedha. Makao yake makuu yapo Dar es Salaam nchini Tanzania.
Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) kimetiliana saini mkataba wa makubaliano juu ya mashirikiano na Chuo Kikuu cha Komoro mjini Moroni katika hafla maalum iliyofanyika tarehe 19 Januari, 2016 na kuhudhuriwa na uongozi wote wa Chuo Kikuu cha Komoro, Balozi wa Komoro nchini Tanzania Dkt. Ahmada El Badaoui Mohamed na Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania nchini Komoro, Bw Mudrik Ramadhan Soragha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mheshimiwa Balozi Seif Ali Idd amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuwa hali ya Zanzibar ni shwari na Wazanzibari wanasubiri kutangaziwa tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi.
Balozi Seif Ali Idd ameyasema hayo Ikulu jijini Dar es salaam leo tarehe 20 Januari, 2016 mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Rais Magufuli.
Soma tamko la serikali juu ya uzushi kuwa Rais Magufuli amepiga marufuku uvaaji wa miniskirt Tanzania
NO BAN ON MINISKIRTS BY PRESIDENT MAGUFULI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kufuatia kifo cha Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) Bi. Asha Bakari Makame kilichotokea jana tarehe 19 Januari, 2016 huko Dubai.