SAUTI- Taarifa ya uchaguzi Zanzibar 20/03/2016
Uchaguzi Zanzibar kufanyika tarehe 20.03.2016
Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imetangaza tarehe ya marudio ya uchaguzi visiwani humo baada ya matokeo ya uchaguzi uliopita kufutwa.
Uchaguzi huo sasa utafanyika Jumapili Machi 20, 2016. Tangazo hilo limetolewa na mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha.
Bw. Jecha amesema tarehe hiyo iliamuliwa na tume baada ya mkutano hapo jana.


















