Home » Node

Serikali Yatoa Ripoti Mwenendo wa Kipindupindu Nchini

SERIKALI kupitia Wizara ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, jinsia, Wazee na Watoto leo imetoa ripoti yake ya wiki juu ya mwenendo wa kipindupindu hapa nchini.

Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam katika ofisi za wazara hiyo, Mkurugenzi wa Huduna za Kinga Nchini, Dk. Neema Rusibamayila amesema kuwa katika kipindi cha wiki moja kuanzia Januari 11 hadi 17,2016 kulikuwa na wagonjwa wapya 549 na vifo 10 huku mikoa iliyoripoti kuwa na ugonjwa ikiongezeka kutoka 11 hadi kufikia 16 ukilinganisha na wiki iliyopita.

TCRA Yavifungia Vituo 27 vya Radio na Televisheni

MAMLAKA ya Mawasiliano TCRA imevifungia vituo 21 vya Radio na 6 vya TV kwa kushindwa kulipa kodi ya lesseni kwa wakati.

Akitangaza uamuzi huo, Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa TCRA Innocent Mungy, amesema vituo hivyo vimefungiwa kwa muda wa miezi mitatu kuanzia Jumatatu ya January 18 mwaka huu na kwamba mitambo ya vituo hivyo itazimwa ifikapo kesho saa 6 usiku (yaani Jumapili usiku kuamkia Jumatatu), na itawashwa baada ya vituo hivyo kulipa madeni yanayowakabili.

CHAN 2016: Guinea 2 Tunisia 2

Timu ya taifa ya soka ya Guinea inayoshiriki katika michuano ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza soka nyumbani CHAN inayoendelea nchini Rwnada, ilitoka nyuma na kusawazisha mabao 2 waliyokuwa wamefungwa na Tunisia katika mchuano wa Kundi C.

Mchuano huo uliochezwa katika uwanja wa Nyamirambo jijini Kigali ulimalizika kwa timu zote mbili kufungana mabao 2 kwa 0.

Hayatoue agawa madaraka

Kaimu rais wa Shirikisho la soka duniani FIFA Issa Hayatoue amesema anakabidhi baadhi ya madaraka ya kuongoza soka barani Afrika.

Uamuzi wa rais huyo wa FIFA ambaye pia ni rais wa Shirikisho la soka barani Afrika CAF, unakuja kuelekea uchaguzi wa kumpata rais mpya wa FIFA mwezi ujao wa Februari.

Raia Marekani walioachiwa huru na Iran wamewasili nchini Ujerumani

Raia watatu wa Marekani walioachiwa huru na utawala wa Iran kama sehemu ya mabadilishano ya wafungwa, wamewasili nchini Ujerumani ambapo wanatarajiwa kusafirishwa hadi kwenye kambi ya kijeshi ya Marekani.

Wafungwa hawa wote walioachiwa wana uraia wa nchi mbili za Iran na Marekani, waliwasili nchini Ujerumani saa chache baada ya kutua kwa muda mfupi mjini Geneva Uswis, ambapo watakuwa Ujerumani kwaajili ya uangalizi wa kiafya kabla ya kurejea nyumbani.

Obama na mwenzake Rouhani, wamepongeza hatua ya kihistoria iliyofikiwa

Rais wa Marekani Barack Obama na mwenzake wa Iran Hassan Rouhani, wamepongeza hatua ya kihistoria iliyofikiwa mwishoni mwa juma ambapo nchi za Magharibi zimetangaza kuiondolea vikwazo vya kiuchumi nchini ya Iran baada ya tangazo la tume ya umoja wa mataifa ya Atomic IAEA kuthibitisha Iran kutimiza masharti ya kupunguza urutubishaji wa

Serikali ya Kenya inasema kuwa operesheni maalumu ya utafutaji na uokoaji

Serikali ya Kenya inasema kuwa operesheni maalumu ya utafutaji na uokoaji inaendelea nchini Somalia siku chache tu baada wanamgambo wa Al-Shabab kutekeleza shambulizi la kushtukiza kwenye kambi moja ya wanajeshi wa Umoja wa Afrika na kudai kuwaua zaidi ya wanajeshi 100.

Kambi hiyo iliyoko kusino magharibi mwa nchi ya Somalia ilivamiwa na wanamgambo hao alfajiri ya siku ya Ijumaa, ikiwa ni shambulio jingine baya zaidi kutekelezwa na wanamgambo hao wakilenga kambi ya wanajeshi wa Umoja wa Afrika.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS