Home » Node

Rais Magufuli amewashukuru Madaktari na Wauguzi wanaomhudumia Mama yake na wagonjwa wengine nchini na amewaombea

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli  tarehe 30 Desemba, 2018 ameungana na Waumini wa Kanisa la Mtakatifu Petro, Parokia ya Oysterbay Jijini Dar es Salaam kuadhimisha sherehe ya Familia Takatifu ya Yesu, Maria na Joseph.

Misa Takatifu ya kuadhimisha sherehe hiyo imeongozwa na Paroko Msaidizi, Padre Bathlomeo Bachoo ambaye amesisitiza umuhimu wa jamii kujenga familia bora, inayochapa kazi na inayomcha Mwenyezi Mungu.

WAANDISHI WA AFRIKA JIFUNZENI KUFICHA MABAYA YENU, TANGAZENI MAZURI KWANI YANAYOENDELEA ULAYA NI HATARI MNO

Usiyoyajua kuhusu maandamano ya Ufaransa

Prof. Dr. Kudret BÜLBÜL

Nchini Ufaransa na katika baadhi ya mataifa ya ulaya kwa mawiki kadhaa sasa tumeshuhudia maandamano makubwa ambayo waliyaita “vizibao vya njano”, tumeshuhudia moto ukiwaka. Vifo pia vilikuwako katika matukio hayo, Nchini Ufaransa mwishoni mwa wiki iliyopita peke yake kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka serikalini mamia ya waandamanaji walijeruhiwa huku maelfu ya waandamanaji wakitiwa nguvuni.

Watanzania wahamasishwa kujitokea kupata chanjo ya Homa ya Ini

Wananchi watakiwa kupima afya zao mara kwa mara kubaini magonjwa mbali mbali nyemelezi ikiwemo ungojwa wa homa ya ini ambao watu wengi bado hawana uelewa nao.

Hayo yamesemwa na Mratibu wa Chanjo ya Homa ya Ini kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dkt Kandali Samuel alipokuwa katika Chuo cha Sayansi ya Afya Cha Mtakatifu Jospeh Jijini Dar Es Salaam wakati wa uchunguzi na utoaji wa chanjo ya homa ya ini kwa wafanyakazi na wanafunzi wa chuo hicho.

Kituo cha afya cha Luchelengwa kupewa gari la kubebea wagonnjwa pamoja na mashine ya kisasa ya Xray

SERIKALI-YAAHIDI-NEEMA-SEKTA-YA-AFYA-RUANGWA

Katika kuhakikisha inawajali wananchi wake na kuboresha huduma za afya nchini, Serikali ya awamu ya Tano imeahidi kukipatia kituo cha afya cha Luchelengwa gari la kubebea wagonnjwa pamoja na mashine ya kisasa ya Xray kabla ya Aprili 2019.

Wananchi wa Kitongoji cha BINYAGO, Kijiji cha Kabegi, Kata ya Ifulifu WAMEAMUA kujenga Shule ya Msingi

Kasi ya Wananchi KUAMUA kuchangia fedha na nguvu zao kwa ajili ya ujenzi wa MIUNDOMBINU ya ELIMU na AFYA imeongezeka sana ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini.

 

Wananchi wa Kitongoji cha BINYAGO, Kijiji cha Kabegi, Kata ya Ifulifu WAMEAMUA kujenga Shule ya Msingi ambayo itaanza kutumika kama ya CHEKECHEA ifikapo April 2019. Lengo ni Shule ya Msingi Binyago ifunguliwe rasmi Januari 2020. Kwa wakati huu Darasa la Chekechea (Utayari) linasomea CHINI ya MTI.

Rais Magufuli aweka jiwe la msingi ujenzi wa daraja jipya la Selander Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 20 Desemba, 2018 ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja jipya la Selander linalounganisha eneo la Aga Khan na Coco Beach Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kupunguza msongamano wa magari katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi.

Daraja hilo lenye urefu wa meta 1,030 na upana  wa meta 20.5 litakuwa na njia 4 za magari na njia 2 za watembea kwa miguu, na litajengwa pamoja na barabara unganishi zenye jumla ya kilometa 5.2.

Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 13 Desemba, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wote wa Tanzania Bara

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 13 Desemba, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wote wa Tanzania Bara, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Pages

Ad
Subscribe to Focus Media RSS